Julai 07, 2014

SOMA HAPA KUHUSU WANAWAKE WALIO WATOROKA BOKO HARAMU

Maafisa wa usalama Nigeria wamesema kuwa zaidi ya wanawake 60 wakiwemo wasichana wa umri mdogo wamewatoroka wanamgambo wa Boko Haram waliokuwa wamewateka nyara.

Wanawake hao wanaaminiwa kuwa miongoni mwa wanawake 68 waliotekwa mwezi uliopita karibu na mji wa Damboa kaskazni mashariki mwa jimbo la Borno.
Baadhi ya vyombo vya habari nchini humo vinadai kuwa huenda wasichana hao walitoroka siku ya Ijumaa, pale watekaji nyara walipokwenda kushambulia kambi ya kijeshi.

Msemaji wa jeshi la Nigeria amesema kuwa Ijumaa hiyo walifanikiwa kuwaua wapiganaji zaidi ya 50 karibu na mji wa Damboa.


Hata hivyo bado wanamgambo hao wa Boko Haram wanawashikilia zaidi ya wasichana wengine 200 waliowateka nyara mwezi Aprili.

BOFYA HAPA KUANGALIA KIPANDE CHA VIDEO MPYA YA DIAMOND PLATNUMZ-Mdogo mdogo.

Julai 06, 2014

NOTI YA 500 SASA KUBADILISHWA KATIKA MFUMO WA SARAFU

Baada ya kuonekana noti ya shilingi 500 ina na mzunguko mkubwa wa matumizi na inachakaa kwa haraka huku kiwango chake cha kuhimili mizunguko ni miezi sita, Benki kuu ya Tanzania (BOT) inatarajia kubadili noti hiyo na kuifanya sarafu.



Sarafu hiyo ya 500 inatarajiwa kutambulishwa na kuanza kutumika July 2014 ikienda sambamba na kipindi cha mwaka huu wa fedha ambapo unaambiwa hii sarafu ikishatoka inatarajiwa kudumu kwenye mzunguko kwa zaidi ya miaka 20 na kubaki na ubora wake uleule, yani ni imara kuliko noti.


Afisa mkuu wa benki kitengo cha idara kurugenzi za kibenki Patrick Fata amekaririwa akisema “Tunafanya hivi kwasababu noti ya 500 inachakaa haraka kulinganisha na mzunguko wake na kuwafikia watu wengi pia huchakaa haraka kutokana na mzunguko wa kushikwa na watu wanaofikia mpaka milioni moja kwa siku, hiyo ni idadi kubwa kuliko ya wanaoshika noti ya elfu 10 kwa siku’